Kwa mujibu wa ripoti ya kitengo cha tarjama cha Shirika la Habari la Hawza, hafla ya kuadhimisha kuuawa kishahidi kwa Ayatollah al-‘Udhma Sayyid Ali Khamenei, kiongozi mkuu wa Mapinduzi ya Kiislamu, iliandaliwa na taasisi za Iran zinazofanya kazi Bangladesh kwa ushirikiano na Baraza la Wanazuoni wa Imamiya wa nchi hiyo pamoja na wadhamini wa Husseinia Kuu ya Mashia wa Dhaka, na kufanyika katika eneo la Husseinia hiyo.
Katika hafla hiyo iliyohudhuriwa na mamia ya Mashia na Masunni wa Dhaka, Rahimi Jahan Abadi, balozi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran nchini Bangladesh, Sayyid Reza Mirmohammadi, mshauri wa utamaduni wa Iran, Hujjatul-Islam wal-Muslimin Sayyid Ibrahim Khalil Rizvi, mkuu wa Baraza la Wanazuoni wa Imamiya wa Bangladesh, na Jamiat al-Mustafa al-Alamiyya kupitia mwakilishi wake mjini Dhaka, walitoa hotuba kuhusu vipengele vya shakhsia na urithi mkubwa na wa kudumu wa miaka 37 ya uongozi wa kiongozi huyo.
Chanzo: Mahusiano ya Umma ya Shirika la Utamaduni na Mawasiliano ya Kiislamu

Maoni yako